maandamano
-
Jeshi la Sepah la Iran: Maadui Wameshindwa, Taifa Liko Imara
Jeshi la Mapambano la Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetaja kushindwa kwa maadui wa Iran katika miongo 47 iliyopita kama ishara ya nguvu, mshikamano wa taifa, na uangalifu wa wananchi. Taarifa hiyo pia inakumbusha changamoto za vikwazo na kipindi cha utegemezi, huku ikihimiza wananchi kushiriki kwa wingi katika maandamano ya kitaifa ya 22 Bahman.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mnamo tarehe 22 Bahman, kwa kuonesha dhamira na msimamo wenu thabiti, muwavunje moyo maadui
Kiongozi wa Mapinduzi amesema kuwa ushiriki wa wananchi katika maandamano ya tarehe 22 Bahman na kuonyesha utii kwa Jamhuri ya Kiislamu ni silaha muhimu ya kuwarudisha nyuma maadui wanaolenga Iran na maslahi ya taifa. Amefafanua kuwa nguvu ya taifa haitokani zaidi na makombora au ndege za kivita, bali inatokana na umoja, fikra, azma na msimamo thabiti wa wananchi.
-
Maandamano Yatikisa Marekani, Minneapolis Kituo Kikuu cha Upinzani Dhidi ya ICE
Wimbi la maandamano linaendelea kuitikisa Marekani, huku jiji la Minneapolis likiwa miongoni mwa vituo vikuu vya upinzani dhidi ya operesheni za polisi wa uhamiaji (ICE). Maelfu ya raia wameingia mitaani wakipinga matumizi ya nguvu kupita kiasi, na maandamano yamesambaa hadi miji mingine kama Portland, Maine, San Francisco na Washington DC. Serikali iko chini ya shinikizo kubwa la ndani, huku wananchi wakidai haki, uwazi na kuheshimiwa kwa utu wa raia.
-
Wakala wa Mossad Akamatwa Iran Wakati wa Maandamano, Mtandao wa Ujasusi wa Mitandao ya Kijamii Wafichuliwa
Vikosi vya usalama vya Iran vimemkamata mtu anayedaiwa kuwa wakala wa Mossad wakati wa maandamano yanayoendelea, kwa tuhuma za kuendesha mtandao wa ujasusi kupitia Instagram. Mamlaka zinasema mtuhumiwa ana uhusiano na shirika lenye makao yake Ujerumani, huku uchunguzi ukiendelea kubaini ukubwa wa shughuli zake.
-
Kuanzia mkusanyiko wa jana hadi hali ya utulivu leo;
waandamanaji wakataa wito wa wapinzani / juhudi za vyombo vya habari vya mapinduzi-pinzan i kupotosha madai halisi
Inaonekana wazi kuwa vyombo vya habari pinzani, hususan mitandao ya Kifarsi inayohusishwa na Wazayuni na Magharibi, kwa makusudi vimeepuka kuzingatia madai halisi ya wafanyabiashara na badala yake vinalenga kuchochea mivutano na machafuko ya kijamii.
-
Madrid itakuwa mwenyeji wa Mahakama ya Umma kuhusu Ushirikiano na Mauaji ya Kimbari ya Wapalestina / Imeitaka Kuvunja Mahusiano na Israel
Katika Siku ya Uunganisho na Palestina, Madrid ilikuwa mwenyeji wa Mahakama ya Umma dhidi ya ushirikiano wa Hispania na pia ikashuhudia maandamano makubwa yaliyoikosoa kukosekana kwa heshima ya mapumziko ya silaha kwa mfumo.
-
Mwanasiasa wa mrengo wa kulia nchini Marekani afungua kesi kwa sababu polisi hawakumuunga mkono katika kitendo cha kuchoma Qur’ani!
Jake Lang, mgombea wa chama cha Republican katika uchaguzi wa Seneti ya Florida na mmoja wa wafuasi wakubwa wa Trump, baada ya kushindwa kutekeleza kitendo cha kuchoma Qur’ani huko Dearborn, jimbo la Michigan, na kuingia katika makabiliano na waandamanaji, amewasilisha kesi ya dola milioni 200 akimshutumu Meya Mwislamu wa jiji hilo na polisi wa eneo hilo kwa “kutompa ulinzi.” Hapo awali, picha zilizochukuliwa na waandishi wa habari huru na vyombo kama Reuters na Anadolu zilionyesha kwamba Lang alijaribu kuchoma nakala ya Qur’ani kwa kutumia kimiminika cha kuwasha moto, lakini alikabiliwa mara moja na mpinga-maandamano aliyemtibua kabla ya kufanya kitendo hicho.
-
Maandamano ya Siku ya Mwenyezi Mungu – 13 Aban yafanyika kwa Hamasa kubwa Mjini Tabriz
Maandamano yalianzia Uwanja wa Saa (Meydan-e Sa’at) na kuendelea hadi Msikiti Mkuu wa Imam Khomeini (r.a), ambapo wazungumzaji mbalimbali walitoa hotuba kuhusu umuhimu wa siku ya 13 Aban (4 Novemba) kama Siku ya Kitaifa ya Mapambano dhidi ya Ubeberu wa Kimataifa.
-
Paul Biya Mwenye Umri wa Miaka 92 Atangazwa Mshindi wa Uchaguzi wa Urais wa Cameroon | Anaendelea Kutawala mpaka afikishe miaka 100
Wafuasi wa upinzani wameishutumu mamlaka kwa “kuiba kura” na wanasisitiza kutambuliwa kwa Bakary kama mshindi halali wa uchaguzi huo.
-
Shambulio dhidi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanazuoni wa Shia wa India
Shambulio hili lilitokea wakati wa kiongozi akiongoza maandamano ya kupinga ujenzi haramu kwenye ardhi ya wakfu ya Karbala Abbas-Bagh, na katika uwepo wa maafisa wa Polisi.
-
Mashambulizi ya maneno kutoka kwa wanaharakati wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali dhidi ya uamuzi wa Uingereza wa kutambua rasmi Palestina.
Uamuzi wa hivi karibuni wa Uingereza kutambua Palestina rasmi umeibua mfululizo wa mwitikio mkali kutoka Marekani na Ulaya.
-
Maandamano Makubwa ya Wenyeji Lebanon Kupinga Uamuzi wa Serikali wa Kuvunja Silaha za Muqawama
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Lebanon wamefanya maandamano na mikutano ya hadhara kupinga uamuzi wa serikali wa kuhodhi na kuvunja silaha za vikosi vya Muqawama.
-
Beirut - Wananchi wa Lebanon Wamiminika Mitaani Kuiunga Mkono Hizbullah na Mapambano ya Muqawama
Wakisambaza ujumbe wao kwa sauti na maandamano, wananchi hao wamesisitiza kuwa Hizbullah si tu harakati ya kijeshi, bali pia ni nguzo muhimu ya taifa katika ulinzi wa mipaka na heshima ya Lebanon. Kwao, wazo la kuondoa silaha za harakati hiyo ni sawa na kuiweka Lebanon mikononi mwa maadui wake.
-
A'shura-Tanzania | Kuelimika Juu ya Tukio la A'shura na Tukio lolote la Historia ya Kiislam ni kusimamia Ukweli Halisi na Haki ilivyo Katika Historia
Tunasoma Matukio ya Historia ya Kiislamu ili Kuelimika na baada ya Kuelimika Tunasimama katika Msingi wa Haki na kusema ukweli Halisi wa Kihistoria ulivyo andikwa katika Vyanzo Sahihi vya Shia na Sunni.
-
Wazayuni wanajutia vita na Iran | Nguvu ya Iran ya Kijeshi sio rahisi kuikabili
Sasa Israel imebakia kujutia na kujilaumu kuingia vitani na Iran na kukiri kuwa Nguvu ya Iran sio rahisi kuikabili. Hii ni baada ya kupata Mashambulizi makali zaidi ya Makombora ya Iran yenye uharibifu mkubwa na milipuko ya kutosha katika kila kona ya Utawala Ghasibu wa Israel.
-
Umati wa Wananchi wa Malaysia wameandamana kuonyesha sapoti yao kwa Iran mbele ya Ubalozi wa Marekani Mjini Kuala Lumpur
Hivi karibuni Dunia itashuhudia Haki ikiishinda batili na Imani ikishinda ukafiri.
-
Maandamano ya “Gaza” Islamabad: Hafidh Naeem atoa wito wa mgomo wa kitaifa na kususia bidhaa za Israel
“Tunaiheshimu nchi yetu, lakini tunataka kuwastua watawala ili wasimame na watu wa Palestina na Kashmir. Ummah wa Kiislamu umelala usingizi wa kutojali.”
-
Morocco; Imeshuhudia Mikusanyiko 105 ya Kuunga Mkono Palestina
Al Jazeera Qatar imeripoti kuwa, (mikusanyiko) maandamano 105 yalifanyika katika miji 58 ya Morocco katika kuwaunga mkono watu wanaodhulumiwa wa Gaza.
-
Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria yalaani Serikali kwa mauaji ya Waandamanaji 26 wanaounga mkono Palestina, na kuwaweka kizuizini 274
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, matukio kadhaa ya amani ya kidini yaliyoandaliwa na Harakati ya Kiislamu ya Nigeria chini ya uongozi wa Sheikh Zakzaky, likiwemo Kongamano la Mwaka la Mauaji ya Zaria ya mwaka 2015 na programu ya Nisfu / Nusu Sha’ban kwa ajili ya kuadhimisha Maulid ya Imam Mahdi (a.t.f.s), yaliripotiwa kuvurugwa na vikosi vya usalama.
-
Takriban watu 20 Wameuawa baada Wanajeshi wa Nigeria kushambulia Maandamano ya Siku ya Quds Mjini Abuja
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.
-
Kulaani Ukandamizaji na Mauaji ya watu wa Nigeria Katika Siku ya Al-Quds | Moto wa Mwamko wa Kiislamu Hautazimika
Baraza la Uratibu wa Tabligh za Kiislamu, limelaani ukandamizaji wa Maandamano ya Siku ya Quds Duniani nchini Nigeria, na limetangaza kuwa: Jinai hizo za kipofu zitazidisha azma ya Mataifa ya Kiislamu kukabiliana ipasavyo na mfumo wa ukoloni na uistikbari.
-
Mwaliko (Wito) wa Ayatollah Ramadhani kwa watu wa Gilan Kushiriki Katika Maandamano ya Siku ya Quds ya 2025
Ayatollah "Reza Ramezani", Mwakilishi wa Wananchi wa Gilan katika Baraza la Wataalamu wa Uongozi, katika Mkesha wa Siku ya Quds Duniani, amewaalika na kuwahimiza watu kushiriki katika Maandamano ya Siku hii.
-
Hazrat Ayatollah Javadi Amoli:
Siku ya Quds ni sehemu ya "Siku ya Kimataifa ya Uislamu"
Ayatollah Javadi Amoli, akiwaalika watu kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alisema: Ni wajibu wetu sote kushiriki katika Maandamano haya, kwanza, Na kila mmoja wetu kwa mujibu wa elimu tuliyo nayo, awe na nia ya Tawalli na Tabarri ya Kimungu, pili, na kujaribu kufayanya kuwa maandamano mapana zaidi, tatu, yaani tuyafanye maandamano haya kwa nia ya kuwa karibu na kuwaheshimu na kuwathamini Mashahidi wa njia hii, ili hatua hizi zote zithibitishwe na Dhati Takatifu ya Mwenyezi Mungu.
-
Ayatollah Makarem Shirazi:
Maandamano ya Siku ya Quds ni Nguvu ya Moyo kwa Mujahidina na Wanyonge wa Palestina na Lebanon
Ayatollah Makarem Shirazi, Miongoni mwa Marjii Taqlid, amewaalika Waislamu ili kushiriki katika Maandamano ya Siku ya Quds, alifafanua akisema: Ni muhimu kwa viongozi na marais wa nchi za Kiislamu kuazimia na kuhakikisha azma yao ya kuacha kutojali na kupuuzia jinai za Wazayuni.
-
Idadi ya waliokamatwa katika Maandamano dhidi ya Serikali ya Uturuki imeongezeka hadi kufikia watu 343
Kufuatia maandamano ya Uturuki yaliyotokana na kukamatwa kwa Meya wa Istanbul, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki ametangaza kukamatwa kwa watu 343 katika majimbo 9 ya nchi hiyo.