Kwa mujibu wa Taarifa ya Shirika la Habari la Ahlulbayt (as) -ABNA-, Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imechukua msimamo kuhusu mabadiliko ya hivi karibuni katika Ukanda wa Ghaza na vita vya mauaji ya kimbari vinavyofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya taifa la Palestina.
Katika taarifa hiyo imesema: Upinzani (Muqawamah) umeanzisha vita vya kuvunjika nguvu kama jibu kwa mauaji ya kimbari dhidi ya raia wasio na hatia, na kila siku wanatumia mbinu mpya za uwanjani kumshangaza adui. Kuongeza mashambulizi ya kijeshi ya wanajeshi wa ukoloni kumesababisha hasara zaidi kwao na kuwapeleka mateka wao kwenye hatima isiyojulikana.
Hamas imesisitiza kuwa "ushindi wa kamili" unaodaiwa na Netanyahu si zaidi ya fikra za uongo zinazowadanganya watu wanaomsikiliza. Hakuna suluhisho linaloweza kupatikana isipokuwa kupitia makubaliano makubwa ambayo Netanyahu anakataa.
Harakati hiyo pia iliongeza kuwa vita ambavyo Netanyahu alitaka viwe vya haraka kumalizika, sasa vimegeuka kuwa mzigo mkubwa na tatizo la kila siku, na kufeli kwa matarajio yake ya kumaliza vita haraka kutakuwa ni mwanzo wa mwisho wa maisha yake ya kisiasa na binafsi.
Your Comment