1 Januari 2026 - 11:07
Osama Hamdan: Kuzungumzia kukabidhi silaha za Muqawama ni jambo lisilo na maana

Katika mwendelezo wa matamko yanayofichua malengo ya kweli ya utawala wa Kizayuni wa Israel, mwanachama mwandamizi wa Harakati ya Hamas, Osama Hamdan, amesisitiza kuwa mazungumzo kuhusu kukabidhi silaha za Muqawama hayana msingi wowote. Ameeleza kuwa wakati Israel inakiuka ahadi zake zote, lengo lake kuu linaendelea kuwa ni kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Mwanachama mwandamizi wa Harakati ya Hamas amesema kuwa lengo la mwisho la utawala wa Kizayuni wa Israel ni kuwahamisha kwa nguvu Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi.

Ameongeza kuwa katika hali ambayo adui wa Kizayuni haheshimu hata moja ya ahadi zake, mazungumzo yoyote kuhusu kukabidhi silaha za Hamas ni ya bure kabisa na ni ndoto isiyo na msingi.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha