Sheikh
-
Sheikh al-Azhar, Ahmad al-Tayeb, amelaani vikali mashambulizi ya uchokozi ya Israel dhidi ya Iran
Kimya cha jumuiya ya kimataifa kuhusu uonevu na uchokozi huu na kukosekana kauli za kuuzuwia, kinachukuliwa kuwa ni ushiriki katika jinai hizo, na matokeo yake pekee yatakuwa ni tishio kwa usalama wa dunia nzima. Vita havizai amani."
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Ziara ya Maulana Sheikh Jalala Hospitali ya Mloganzila kumtembelea Sheikh Mbelango Allah aimarishe Afya yake
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ampe afueni ya haraka na amuwekee wepesi katika kila jambo. Uwepo wake ni hazina kwa Uislamu na Waislamu.
-
Sheikh Abdul Ghani Khatibu | Maisha bila Malengo, ni Maisha yasokuwa na maana
Tukumbuke, maisha haya ni safari. Safari bila ramani hupotea. Weka malengo yako, yashike kwa mikono miwili, na muombe Allah akukadirie kheri na mafanikio ndani yake.
-
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dr.Abubakar Zubair bin Ally, asisitiza umuhimu wa Elimu ya Dini ya Kiislamu
Elimu ya dini ni muhimu kwa msingi wa maadili mema, lakini haiwezi kuchukua nafasi ya elimu ya dunia katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya taifa. “Tunapaswa kuwa na masheikh na maimamu, lakini pia tuwe na madaktari, wahandisi na wanasayansi,”.
-
Chuo Kikuu cha Jamiatul Mustafa - Dar-es-salaam - Tanzania kimeandaa Kongamano la Kisayansi kuhusu Maendeleo katika Ulimwengu wa Kiislamu
Kongamano hili litajadili juu ya Maendeleo katika Ulimwengu wa Kiislamu kati ya changamoto na mkakati. Mhadhiri: Samahat Sheikh Mulaba Saleh. Siku ya: Jumamosi; 19/04/2025. Kuanzia: 10 - 12:00 AM. Katika Ukumbi wa Sala wa Chuo cha Jamiat Al- Mustafa. Watu wote mnakaribishwa kuhudhuria katika nad'wa hii ya Kisayansi.
-
Samahat Sheikh Kadhim Abbas, Mudir wa Hawza za Bilal Muslim Tanga - Tanzania, amefanya ziara muhimu katika Hawza ya Imam Ali (a.s)
Sheikh Kadhim ametoa akitoa nasaha kwa nasaha kwa Wanafunzi amesema: "Wanafunzi wa Kidini wanapaswa kusoma kwa bidii na kuzingatia masomo yao ili kuhakikisha wanayafikia malengo matukufu ya kuchuma Elimu na Maarifa ya Dini Tukufu ya Kiislamu".
-
Sheikh Izzud_Din wa Kenya:
Nakiri kwa sababu nilipotezwa na hisia zangu, naomba radhi na msamaha
"Natumia fursa hii kumuomba radhi Rais wa Tanzania, Dr.Samia Suluhu Hassan kwa kumhusisha katika mazungumzo yangu".
-
Siku ya Quds Duniani:
Kongamano la Siku ya Quds Duniani lilifanyika Jijini Tanga, Tanzania
Kuna umuhimu Mkubwa kwa Waislamu na Watu wote huru na wapenda Haki Duniani, kuzidi kusimama pamoja na wadhulumiwa wa Palestina na kutetea Haki za watu wote wanyonge popote pale walipo Duniani. Watu mbalimbali kutoka Jiji la Tanga walihudhuria katika Mkusanyiko huu wa kuhuisha Siku ya Kimataifa ya Quds, wakiwemo Viongozi wa Taasisi mbalimbali za Kidini na Madhehebu mbalimbali.
-
Njia ya Dhambi Huanza na Dakika ya Uzembe
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atujaalie sote tupate taufiki ya kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), kwani wao ndio Njia iliyonyooka, na atakayeshikamana nao wao na Qur'an Tukufu, huyo ataepukana na upotevu, kwa sababu wao ndio sehemu ya Kizito cha pili baada ya Qur'an Tukufu, na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) ametuusia katika Hadithi Sahih na Mutawatiri ya Thaqalayni, kushikamana na Ahlul-Bayt (a.s) na Quran Tukufu ili tuje kupotea baada yake.
-
Mayahudi shari ndio chaguo lao, na kuangamizwa ndio hatima yao
Sheikh Mselem: "Mayahudi walikuwepo Madina. Lakini walileta ukorofi na kibri, wakawa wakivunja makubaliano waliyokuwa wakiingia na Mtume (s.a.w.w). Mtume (s.a.w.w) akawatandika na kuwatimua kutoka katika Bara Arabu">