Shia
-
Mkutano wa wapinzani wa kisiasa wa Taliban nchini Pakistan: Kuunda serikali ya pamoja kutasaidia amani na utulivu wa Afghanistan
Mkutano wa baadhi ya wapinzani wa kisiasa wa serikali ya Taliban ukiwa na kaulimbiu ya “Kuelekea Umoja na Uaminifu” umefanyika kwa siku mbili mjini Islamabad, mji mkuu wa Pakistan. Katika mkutano huu, baadhi ya wasichana wa Shia, wakiwemo Zahra Joyaa, mwanahabari maarufu kutoka Afghanistan, pia walihudhuria.
-
Mkutano wa Viongozi wa Iran na Iraq:
Pezeshkian: Waislamu wafanye jitihada kusitisha jinai za utawala wa Kizayuni Al-Sudani: Juhudi za nchi za Kiislamu zisibaki kwenye matamko tu
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Waziri Mkuu wa Iraq wametoa msisitizo juu ya ulazima wa kuchukua msimamo mmoja wa pamoja kati ya nchi za Kiislamu, ili kuwe na hatua madhubuti na za vitendo za kusitisha na kuzuia marudio ya jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Ayatollah Ashrafi Shahroudi alipokutana na viongozi wa Shirika la Habari la “Abna” alisema:
"Kuonyesha huruma na kujali kwa ajili ya mafundisho ya Ahlul Bayt (a.s) huleta maendeleo katika kazi mbalimbali"
"Kwa juhudi za Imam na Mapinduzi, jina la Ahlul Bayt (a.s) limejulikana na kutambulika kote duniani. Sababu kuu ya uadui wote wa naadui dhidi ya IRAN, unatokana na IRAN na Jamhuri ya Kiislamu kuzingatia na kufuatilia zaidi mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s). Kuanzia vita vya miaka minane hadi fitina ya Daesh na hata uvamizi huu wa utawala wa Kizayuni ni kwa sababu ya imani ya dhati ya Taifa la Iran na uvumilivu wa Mashia."
-
Jeshi la Lebanon limepokea silaha nzito kutoka kwenye kambi za Wakpalestina
Jeshi la Lebanon limeanza mchakato wa kupokea silaha kutoka kwenye Kambi za Wapalestina katika Mji wa Sur Kusini mwa nchi hiyo.
-
Kiongozi wa Kiislamu wa Shia Pakistan:
Hali ya Gilgit-Baltistan Ni Mbaya Sana; Watawala Ni Kama Adhabu Inayowakalia Wananchi
Kiongozi huyo wa kidini wa Shia Pakistan alisisitiza kuwa leo hii, rushwa, ukosefu wa sheria na usimamizi mbovu ndizo zimeenea kote katika eneo la Gilgit-Baltistan. “Wananchi wanajiona wapo peke yao, wamenyimwa haki na hawana pa kutegemea. Endapo hali hii itaendelea, ghadhabu ya wananchi inaweza kubadilika na kuwa dhoruba kubwa ambayo mzigo wake utabebwa na watawala pekee,”
-
Kuuawa na kujeruhiwa kwa Waislamu 5 wa Kishia nchini Pakistan katika shambulio la kundi la kitakfiri la Sipah-e-Sahaba
Waislamu wawili wa Kishia wameuawa shahidi katika shambulio la kigaidi lililotokea katika jiji la Karachi, Pakistan.
-
Jumuiya ya Waislamu wa Shia Khoja Ithna Ashari Jamiat katika Matembezi ya A'shura
ASHURA ni siku ya kumi ya mwezi mtukufu wa Muharram. Katika siku hii ya Ashura mjukuu wa Mtume yaani Imam Hussain (as) aliuawa katika tambarare za mji wa Karbala baada ya kusimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu , utu pamoja na kupigania uislamu.
-
Himaya thabiti ya Allama Sajid Naqvi kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi/Syed Khamenei Shkhsia wa Kimataifa anayeheshimika katika Ulimwengu wa Kiislamu
Akikosoa matamshi ya hivi karibuni ya kimatusi dhidi ya Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema kuwa, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni Shakhsia mwenye hadhi ya Kimataifa katika Umma wa Kiislamu, na kauli yoyote ya kumtusi inaweza kuwa na matokeo mabaya na ya kutia wasiwasi.
-
Mimbari ya Imam Hussein (as) - Nchini Malawi | "Tofauti kati ya Mtu anayemjua Imam Hussein (AS) na Asiyemjua Imam Hussein (as)"
Sheikh Abdul Rahman Kachere: "Mtu anayemfahamu Imam Hussein (AS) daima ni jasiri katika kukabiliana na dhulma".Kumjua vizuri Imam Hussein (as) kutawafanya watu wa mataifa mbalimbali kumpinga adui na dhalimu, na kutambua njama za adui na dhalimu dhidi ya mataifa yao, na kuwa tayari kupambana kwa ajili ya kuinusuru Haki, kwa ajili ya kuondoa uistikbari, dhulma na unyonyaji wa mfumo mpya wa ukoloni unaoitwa: Ukoloni mambo leo.
-
Mikakati ya Imam Hadi (a.s) katika Kueneza Mtandao wa Shi'a na Kuimarisha Harakati za Kijamii
Shughuli za Imam Hadi (a.s) zilikuwa na nafasi muhimu katika kuhifadhi utambulisho wa kiakili na imani wa Waislamu wafuasi wa Madhehebu ya Shi'a Ithna Ashari. Uongozi wake wa kiroho na wa fikra kwa Shi'a waliokuwa Samarra, kuimarisha mtandao wa mawasiliano kati ya wafuasi wa Ahlul Bayt(as), na kusimama imara dhidi ya shinikizo la wa Abbasi, ni miongoni mwa huduma muhimu za Imamu Hadi katika maandalizi ya Shi'a kwa zama za Ghaibat Kubwa (Kutoonekana kwa Muda Mrefu).
-
Saumu ya Arafa | Kwa Mujibu wa Madhehebu ya Shia Ithna Ashari: "Kufunga Siku ya Arafa ni Sunna na si wajibu"
Hoja na Dalili Juu ya Sunna ya Saumu ya Siku ya Arafa: Riwaya kadhaa za Kishia zinaelezea fadhila za kufunga Siku ya Arafa, kama vile riwaya ya Abdur_Rahman bin Abi Abdillah kutoka kwa Abul Hassan (as).
-
Kufanyika kwa Tamasha la Ushairi wa Amani katika mji wa Parachinar, Pakistan / Mkutano wa washairi wa Kishia na Kisunni wenye ujumbe wa umoja
Washairi Mashuhuri wa Kishia na Kisunni kutoka maeneo yote ya Kurram wamekusanyika katika tamasha lenye mada ya amani lililofanyika katika mji wa Parachinar, Pakistan.
-
Mkutano na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batlida Burian, pamoja na baadhi ya Masheikh wa Kishia na Kisunni.
"Tanga ni mfano wa kuigwa kwa utulivu wa kidini. Tuendelee kudumisha hali hii na kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya jamii yetu."
-
Makala Fupi Kuhusu Kuzaliwa kwa Sayyidat Fatima Maasoumeh (sa) | Imam Ridha (as) alisema: "Yeyote atakayemzuru Fatima Maasoumeh Qom, atapata Pepo."
Fatima Maasoumeh (sa) alikuwa mashuhuri kwa elimu yake, ibada, na ufasaha. Alifuatilia harakati za kaka yake, Imam Ridha (as), na alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki na kufichua dhulma za watawala wa wakati huo. Katika safari yake ya kuelekea Khurasan kumtembelea kaka yake aliyehamishwa kwa nguvu na Khalifa Ma’mun, Sayyidat Fatima alifika mji wa Qom (Iran ya leo), ambako alipata maradhi mazito na kufariki dunia tarehe 10 Rabi'ul Thani mwaka 201 Hijria. Alizikwa mjini Qom, ambao baadaye ukawa kituo muhimu cha elimu ya Kiislamu.
-
Matendo Mema katika Dua na Swala za Sunna (Sehemu ya 1)
Huu ni mkusanyiko uliokusanya baadhi ya matendo ya kufanya usiku na mchana, swala za Sunnah zilizopokewa, ponyo, kinga, dhikir, dua za ajabu, athari za baadhi ya Aya na ufupisho wa kuwafanyia adabu waliokufa, nimezikusanya ili niziambatanishe kwenye Mafatihul Jinani kisha kitabu kikamilike kwa njia zote na iwe na manufaa kwayo yaliyotimia.
-
Siku ya Wakati Maalum:
Ni ipi Maana ya Kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema kumwambia Shetani: "یوم الوقت المعلوم" “Siku ya Wakati Maalum"
katika ufahamu wa Shia (Wafuasi wa Ahlul-Bayt - a.s - ), "یوم الوقت المعلوم" ni Siku ya dhahiri ya Haki na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Duniani, yaani Siku ya Mapinduzi ya Dunia yakiongozwa na Imam Mahdi (a.t.f.s), kabla ya Siku ya Kiyama.
-
Hadithi / Tukio la Kushusha Bendera ya Kuba ya Haram ya Bibi Zainab (a.s)
Imam wa Haram ya Bibi Zainab (a.s) alitangaza sababu ya kushushwa kwa bendera iliyokuwa juu ya Kuba ya Haram hiyo Tukufu.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu:
Udhalilishaji wa hivi karibuni wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni una nyanja tata zaidi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kudumisha Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu akilaani udhalilishaji wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni alisema: Udhalilishaji wa hivi karibuni una nyanja tata zaidi, na inatarajiwa kutoka kwa viongozi wa masuala haya kuchukua hatua za kuzuia kurudiwa kwa maafa kama haya.
-
Ukabidhi wa Hiari wa Silaha Parachinar; Hatua Muhimu kuelekea Amani Endelevu
Baada ya utekelezaji wa Mkataba wa Amani wa Kohat, Waislamu wa madhehebu ya Shia katika wilaya ya Kurram, eneo la Parachinar nchini Pakistan, wamekabidhi silaha zao kwa hiari kwa wawakilishi wa jeshi na maafisa wa serikali ya Pakistan ili kuonesha nia yao ya kutafuta amani.
-
Wakimbizi wapya 13,000 wa Syria wamekimbilia Lebanon / wakikimbia uhalifu wa Al-Julani kwenye Pwani ya Syria
Takriban wakimbizi wapya elfu 13 wa Syria wameingia katika vijiji na miji 23 Kaskazini mwa Lebanon.
-
Imetolewa Katika Mkutano wa Ukosoaji wa Mfululizo wa Muawiyah:
Mfululizo wa filamu ya “Muawiyah”, Ni utekelezaji wa amri za Kiwahabi / Ili kuvutia hadhira badala ya kusimulia Historia halisi!
Katika mkutano wa mapitio ya mfululizo wa filamu ya “Muawiyah”, wataalamu walizingatia lengo kuu la mfululizo huu kuwa ni utakaso wa Bani Umaiyya na Muawiyah, na ni upotoshaji wa Historia kwa kupendelea Uwahabi, na ni katika kukamilisha mradi wa migogoro baina ya Shia-Sunni.
-
Swali kuhusu kadhia ya Palestina:
Ni kwa nini Mashia tu ndio wako mstari wa mbele kwenye kulitetea suala la Palestina?!
Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge: "Uislamu usiokuwa wa Ahlulbayt wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), huo umetengenezwa na Mayahudi au kama haukutengenezwa na Mayahudi basi umeingizwa mikono kwa asilimia 99% na Mayahudi".