Shia
-
Makala Fupi Kuhusu Kuzaliwa kwa Sayyidat Fatima Maasoumeh (sa) | Imam Ridha (as) alisema: "Yeyote atakayemzuru Fatima Maasoumeh Qom, atapata Pepo."
Fatima Maasoumeh (sa) alikuwa mashuhuri kwa elimu yake, ibada, na ufasaha. Alifuatilia harakati za kaka yake, Imam Ridha (as), na alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki na kufichua dhulma za watawala wa wakati huo. Katika safari yake ya kuelekea Khurasan kumtembelea kaka yake aliyehamishwa kwa nguvu na Khalifa Ma’mun, Sayyidat Fatima alifika mji wa Qom (Iran ya leo), ambako alipata maradhi mazito na kufariki dunia tarehe 10 Rabi'ul Thani mwaka 201 Hijria. Alizikwa mjini Qom, ambao baadaye ukawa kituo muhimu cha elimu ya Kiislamu.
-
Matendo Mema katika Dua na Swala za Sunna (Sehemu ya 1)
Huu ni mkusanyiko uliokusanya baadhi ya matendo ya kufanya usiku na mchana, swala za Sunnah zilizopokewa, ponyo, kinga, dhikir, dua za ajabu, athari za baadhi ya Aya na ufupisho wa kuwafanyia adabu waliokufa, nimezikusanya ili niziambatanishe kwenye Mafatihul Jinani kisha kitabu kikamilike kwa njia zote na iwe na manufaa kwayo yaliyotimia.
-
Siku ya Wakati Maalum:
Ni ipi Maana ya Kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema kumwambia Shetani: "یوم الوقت المعلوم" “Siku ya Wakati Maalum"
katika ufahamu wa Shia (Wafuasi wa Ahlul-Bayt - a.s - ), "یوم الوقت المعلوم" ni Siku ya dhahiri ya Haki na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Duniani, yaani Siku ya Mapinduzi ya Dunia yakiongozwa na Imam Mahdi (a.t.f.s), kabla ya Siku ya Kiyama.
-
Hadithi / Tukio la Kushusha Bendera ya Kuba ya Haram ya Bibi Zainab (a.s)
Imam wa Haram ya Bibi Zainab (a.s) alitangaza sababu ya kushushwa kwa bendera iliyokuwa juu ya Kuba ya Haram hiyo Tukufu.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu:
Udhalilishaji wa hivi karibuni wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni una nyanja tata zaidi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kudumisha Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu akilaani udhalilishaji wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni alisema: Udhalilishaji wa hivi karibuni una nyanja tata zaidi, na inatarajiwa kutoka kwa viongozi wa masuala haya kuchukua hatua za kuzuia kurudiwa kwa maafa kama haya.
-
Ukabidhi wa Hiari wa Silaha Parachinar; Hatua Muhimu kuelekea Amani Endelevu
Baada ya utekelezaji wa Mkataba wa Amani wa Kohat, Waislamu wa madhehebu ya Shia katika wilaya ya Kurram, eneo la Parachinar nchini Pakistan, wamekabidhi silaha zao kwa hiari kwa wawakilishi wa jeshi na maafisa wa serikali ya Pakistan ili kuonesha nia yao ya kutafuta amani.
-
Wakimbizi wapya 13,000 wa Syria wamekimbilia Lebanon / wakikimbia uhalifu wa Al-Julani kwenye Pwani ya Syria
Takriban wakimbizi wapya elfu 13 wa Syria wameingia katika vijiji na miji 23 Kaskazini mwa Lebanon.
-
Imetolewa Katika Mkutano wa Ukosoaji wa Mfululizo wa Muawiyah:
Mfululizo wa filamu ya “Muawiyah”, Ni utekelezaji wa amri za Kiwahabi / Ili kuvutia hadhira badala ya kusimulia Historia halisi!
Katika mkutano wa mapitio ya mfululizo wa filamu ya “Muawiyah”, wataalamu walizingatia lengo kuu la mfululizo huu kuwa ni utakaso wa Bani Umaiyya na Muawiyah, na ni upotoshaji wa Historia kwa kupendelea Uwahabi, na ni katika kukamilisha mradi wa migogoro baina ya Shia-Sunni.
-
Swali kuhusu kadhia ya Palestina:
Ni kwa nini Mashia tu ndio wako mstari wa mbele kwenye kulitetea suala la Palestina?!
Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge: "Uislamu usiokuwa wa Ahlulbayt wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), huo umetengenezwa na Mayahudi au kama haukutengenezwa na Mayahudi basi umeingizwa mikono kwa asilimia 99% na Mayahudi".