Waislamu
-
Imani ya Mahdawi: Vipi Iliwafanya Waislamu wa Kishia Kusimama Imara Katika Mitihani Mikubwa ya Ulimwengu wa Kiislamu?
Madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s), likiwa limejengwa juu ya itikadi ya kumwamini Imam Mahdi (a.t.f.s) aliyeahidiwa kwa mataifa yote, linabeba mafundisho yenye utajiri mkubwa kuhusu uadilifu na uokovu. Mafundisho haya yamewafanya Waislamu wa Kishia kubaki imara, thabiti na wenye heshima katika mitihani na misukosuko mikubwa ya ulimwengu wa Kiislamu.
-
Qalibaf:
Hakuna nchi yoyote ya Kiislamu inayopaswa kuwa na uhusiano wowote na adui wa Uislamu na Waislamu
Spika wa Bunge alisema: Marekani inawagawa umma wa Kiislamu katika pande mbili — upande mmoja ambao unapaswa kushambuliwa na kukaliwa, na upande mwingine ambao unapaswa kukubali “Amani ya Ibrahimu” na kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni. Hakuna nchi yoyote ya Kiislamu inapaswa kujiruhusu kuanzisha uhusiano na adui wa Uislamu na Waislamu.
-
Mhubiri Mashuhuri wa Pakistan: Msiba wa Gaza ni mtihani wa imani na dhamiri ya Taifa la Kiislamu
Mmoja wa wanazuoni wa Kishia kutoka Pakistan amesisitiza kuwa: Licha ya kuwepo Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani, ummah haujafanikiwa kutekeleza jukumu lile ambalo Qur’an na Sharia zinatarajia kutoka kwake, na hili lenyewe ni ishara ya kushindwa kwa pamoja kwa umma wa Kiislamu.
-
Katika Kikao cha "Nafasi ya Wanawake wa Vyombo vya Habari katika Muqawama (Mapambano - Upinzani) ilibainika:
Kutoka kwa Zainab al-Kubra(s) hadi leo; Karbala ni Chuo cha Habari cha Mwanamke Muumini /Wanawake Waislamu wako mstari wa mbele katika vita vya Habari
Misingi Mitatu ya Wajibu wa Mwanamke Mwislamu katika Ulimwengu wa Habari Kueneza uelewa: Mwanamke Mwislamu anapaswa kuwa sauti ya ukweli, afichue upotoshaji wa vyombo vya habari vya upande wa uongo, na atangaze mateso ya waliodhulumiwa duniani – kuanzia Palestina hadi kila sehemu inayokandamiza utu. Kutetea utambulisho: Vyombo vya habari vya kisasa vinajaribu kumvua mwanamke heshima yake na kumgeuza bidhaa ya matangazo. Mwanamke Mwislamu lazima athibitishe kuwa uhalisia na usasa vinaweza kuishi pamoja, na kwamba heshima hupimwa kwa utiifu wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu, si kwa uchi au mvuto wa sura. Kulea kizazi cha waandishi wa kweli: Wajibu wa mwanamke hauishii katika kushiriki binafsi katika vyombo vya habari; anatakiwa kulea kizazi kinachotambua nguvu ya neno na dhamana ya uandishi wa ukweli.
-
Waabudia Ng'ombe dhidi ya Wauzaji wa nyama ya Ng'ombe:
Mashambulizi ya wapiganaji wa Kihindu dhidi ya duka la Waislamu katika Jimbo la Maharashtra
Baadhi ya wanachama wa kundi la msitari wa “Bajrang Dal” katika Jimbo la Maharashtra, India, walivamia duka la nyama la Waislamu huku wakipiga kelele za dhihirisho la chuki dhidi ya Uislamu na wakilaumu wafuatiliaji wa mauzo ya nyama ya ng’ombe.
-
Sheikh wa Kisunni Lebanon: Tukisikia Hizbullah inataka kuweka silaha chini, sisi Wasunni tutapinga vikali
Sheikh Maher: Kuwasilisha (kukabidhi) silaha ni usaliti; usaliti kwa Mungu na Mtume (s.a.w) na sisi tunaelewa kabisa hilo.
-
Hispania: Waislamu na wahamiaji wana jukumu muhimu katika uchumi na usalama wa kijamii
Serikali ya Hispania imeonyesha katika ripoti yake, huku ikikanusha imani za makundi ya mrengo wa kulia mkali, kwamba Waislamu na wahamiaji wameshiriki vizuri katika jamii ya nchi hiyo na wana mchango mkubwa katika uchumi na kuhakikisha usalama wa kijamii, ingawa bado wanakabiliana na ubaguzi katika baadhi ya maeneo kama upatikanaji wa makazi.
-
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad: Israel na Trump wamesalimu amri mbele ya masharti ya Muqawama huko Gaza
Ayatollah Sayyid Yasin Musawi, Imamu wa Ijumaa wa Baghdad na mmoja wa wasomi mashuhuri wa Hawza ya Najaf Ashraf, amesisitiza kuwa “tukio muhimu zaidi duniani kwa sasa ni kusalimu amri kwa Israel na Waziri Mkuu wake Benjamin Netanyahu pamoja na Rais wa Marekani Donald Trump mbele ya masharti ya Muqawama wa Kiislamu huko Gaza.” Amesema kuwa usitishaji mapigano uliotangazwa hivi karibuni ni “ushindi wa wazi wa Muqawama na matokeo ya uimara wa wananchi wa Palestina.”
-
Ayatullah Nuri Hamedani: Leo, jambo kubwa zaidi la ma’rufu ni umoja kuzunguka mhimili wa Uongozi wa Mapinduzi na kulinda Mfumo wa Kiislamu
Ayatullah Nuri Hamedani amesisitiza kuwa: Kwa uwazi tunatambua kwamba Amr bil Ma’ruf na Nahy anil Munkar ni kati ya wajibu muhimu zaidi wa Kiislamu — au ndio wajibu muhimu zaidi — na hilo peke yake linatosha kuonyesha hadhi ya juu ya wajibu huu, hivyo haipaswi kuuchukulia kuwa jambo dogo.
-
Ayatollah Sayyid Yasin Musawi, Imamu wa Ijumaa Baghdad:
Jeshi la Muqawama chini ya Bendera ya Wilayat litaendeleza njia ya Shahidi Nasrallah | Umoja na utiifu kwa Kiongozi wa Kiislamu ni sharti la ushindi
Ayatollah Musawi alisisitiza kuwa jina “Nasrallah” lina mizizi katika nusra ya Mwenyezi Mungu, na historia ya mapambano imethibitisha kuwa licha ya gharama kubwa, irada ya umma kuendeleza njia ya mashahidi na kufikia ushindi haitadhoofika kamwe.
-
Kiongozi wa kidini wa Waislamu wa Sunni nchini Afghanistan;
Amekosoa sera za Taliban dhidi ya wanawake, akisema: «Mwanamke ni shujaa na ndiye anayezalisha mashujaa wengine»
Hali ilivyo sasa ambapo Taliban nchini Afghanistan wamepunguza haki za wanawake na wasichana kuhusiana na elimu, kazi, na ushiriki katika jamii, kiongozi mmoja wa dini wa Sunni amekosoa waziwazi sera za kutozingatia wanawake za Taliban katika hotuba yake ya umma.
-
Mashambulizi ya maneno kutoka kwa wanaharakati wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali dhidi ya uamuzi wa Uingereza wa kutambua rasmi Palestina.
Uamuzi wa hivi karibuni wa Uingereza kutambua Palestina rasmi umeibua mfululizo wa mwitikio mkali kutoka Marekani na Ulaya.
-
Waislamu wawili kati ya watatu nchini Ufaransa ni waathirika wa ubaguzi wa rangi
Chuki dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa inaongezeka, na asilimia 66 ya Waislamu wa nchi hiyo wamekuwa waathirika wa ubaguzi na chuki za kijinsia na kikabila katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
-
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan: Osama bin Laden alikuwa zao la Amerika / Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuunda Muungano sawa na NATO
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan alisema: "Shambulio la Israel dhidi ya Qatar lilifanyika kwa ridhaa ya Amerika, na Waislamu wanapaswa kuelewa ukweli huu na kutofautisha kati ya "Marafiki bandia na maadui wa kweli."
-
Mkutano wa Dharura wa Viongozi wa Nchi za Kiislamu na Jumuiya ya Kiarabu huko Doha:
Pezeshkian: Uvamizi dhidi ya Qatar ni shambulio dhidi ya diplomasia ya kimataifa / Umoja wa Waislamu ndiyo njia pekee ya kukabiliana na uvamizi huu
Rais wa Iran, Dkt. Masoud Pezeshkian, akilaumu kitendo cha kigaidi na jinai cha utawala wa Kizayuni katika shambulio la mji mkuu wa Qatar siku za hivi karibuni, alisema: “Kwa bahati mbaya, magaidi wanaotawala Tel Aviv, wakijiona hawana hatia baada ya udanganyifu wa aina ile ile kwenye diplomasia Juni 2025 na kuanzishwa kwa vita vya uvamizi dhidi ya watu wa nchi yangu, walijitahidi zaidi.”
-
Kiongozi wa Ansarullah: Kuwasaidia Wapalestina Wanaodhulumiwa Ni Wajibu wa Mataifa ya Kiislamu
"Mara tu matatizo ya Waislamu yanapoanza, basi hilo huwa ni matokeo ya kugeuka mbali na Qur’an na mwongozo wa Mtume. Suluhisho la kweli ni kurejesha uhusiano wa dhati na Qur’an na Sunnah ya Mtume (s.a.w.w).”
-
Mgogoro wa marufuku ya Hijabu katika mji wa “Axum” nchini Ethiopia / Wanafunzi Waislamu warejea shuleni kwa amri ya mahakama
Katika nchi yenye historia ya kuishi kwa amani baina ya dini mbalimbali, mgogoro wa hijabu katika mji wa Axum umeibua tena mjadala kuhusu uhuru wa kidini nchini Ethiopia. Uamuzi wa hivi karibuni wa Mahakama Kuu ya eneo la Tigray unaweza kuwa hatua muhimu katika kuthibitisha haki za Waislamu na kuimarisha msingi wa usawa wa uraia .
-
Abdulmalik al-Houthi Awashutumu Waislamu Bilioni Mbili kwa “Kukaa Kimya” Kuhusu Matukio ya Gaza
Katika hotuba yake, al-Houthi alieleza kwa masikitiko na ghadhabu hali ya “kutochukua hatua” kwa Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani, akisema kuwa ukimya huo ni “aibu na fedheha” inayoweza kuleta madhara si tu kwa Palestina, bali pia kwa ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
“Msikiti; Kitovu cha Umoja na Ngome ya Mapambano” Kaulimbiu ya Siku ya Kimataifa ya Msikiti
Tehran – Katibu wa Kituo cha Kitaifa cha Msikiti, Hujjatul-Islam Ali Nouri, ametangaza kuwa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Msikiti mwaka huu yatafanyika kuanzia tarehe 31 Mordad hadi 7 Shahrivar (sawa na 22–29 Agosti 2025) katika ngazi ya kitaifa, mikoa na wilaya, chini ya kaulimbiu: “Msikiti, Kitovu cha Umoja, Ngome ya Mapambano.”
-
Mazuwwari wa Afghanistan: Warithi wa Karbala, Sio Vipande vya Mchezo wa Chesi
Ukosoaji wa Matusi ya Gazeti la Ettelaat-e-Rooz dhidi ya Waislamu wa Kishia wa Afghanistan
Katikati ya wimbi la maandiko yenye upendeleo ambayo, kwa kisingizio cha utafiti, yanadhalilisha imani na uelewa wa Waislamu wa Kishia wa Afghanistan, ni lazima kukumbusha ukweli: ukweli wa uhusiano wa kihistoria na wa kina kati ya mataifa mawili ya Iran na Afghanistan, ambao katika nyanja za mapambano, ulinzi na mshikamano, daima wamesimama bega kwa bega — na lengo la pamoja la maadui wao limekuwa kuvunja mshikamano huu.
-
Kuuawa na kujeruhiwa kwa Waislamu 5 wa Kishia nchini Pakistan katika shambulio la kundi la kitakfiri la Sipah-e-Sahaba
Waislamu wawili wa Kishia wameuawa shahidi katika shambulio la kigaidi lililotokea katika jiji la Karachi, Pakistan.
-
Waduruze - Asili, Itikadi na Ushirikiano wao na Maadui wa Ummah wa Kiislamu (Israel + Marekani)
Katika siku za karibuni, kundi hili limeripotiwa kuhusika katika mauaji ya Waislamu huko Suwayda, Syria, kwa usaidizi wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Waduruze wanajulikana kuwa na uhusiano wa karibu na jeshi la Israel, ambapo vijana wao wengi wanahudumu humo.
-
Jumuiya ya Waislamu wa Shia Khoja Ithna Ashari Jamiat katika Matembezi ya A'shura
ASHURA ni siku ya kumi ya mwezi mtukufu wa Muharram. Katika siku hii ya Ashura mjukuu wa Mtume yaani Imam Hussain (as) aliuawa katika tambarare za mji wa Karbala baada ya kusimama kidete dhidi ya mtawala dhalimu wa wakati ule, Yazid bin Muawiya, akatoa fundisho la kukataa kumpigia magoti mdhalimu huyo, ndipo akajitolea maisha yake, akauawa ili kunusuru ubinaadamu , utu pamoja na kupigania uislamu.
-
Fat'wa Muhimu na Wazi ya Ayatollah Makarem Shirazi Dhidi ya Viongozi wa Kizayuni na Ubeberu
Ni wajibu kwa Waislamu kote duniani kuwafanya maadui hawa wajute kwa matamshi na vitendo vyao. Na ikiwa Waislamu watapata mashaka au hasara kutokana na kusimama dhidi yao, basi wao watakuwa na thawabu ya mujahid (mpiganaji katika njia ya Mwenyezi Mungu), Insha'Allah.
-
Imam Khomein Akumbukwa: Mamia Wahudhuria Maadhimisho ya Kifo Chake Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam
Imam Khomein (ra) anakumbukwa duniani kote kama mtetezi wa wanyonge, hususan kwa msimamo wake thabiti katika kuwatetea Waislamu wa Palestina na wananchi wa Palestina kwa ujumla.
-
Mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza yaendelea wakati Waislamu wakiadhimisha Eid al-Adha huku ikinukia harufu ya damu
Sambamba na maadhimisho ya Sikukuu ya Eid al-Adha, Ukanda wa Gaza kwa mara nyingine umeshuhudia mashambulizi makali na ya umwagaji damu kutoka kwa jeshi la utawala wa Kizayuni.
-
Waziri Mkuu wa Uingereza ametuma salamu za pongezi kwa Waislamu kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Adha
Baadhi ya viongozi wa kisiasa wa Uingereza, wakiwemo Waziri Mkuu wa nchi hiyo, wametuma salamu za pongezi kwa Waislamu wa Uingereza na ulimwenguni kote kwa mnasaba wa Sikukuu ya Eid al-Adha.
-
Kiongozi wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Watu wa Gilgit-Baltistan hawatakaa kimya mbele ya dhulma; hata wakikata shingo zetu au kukata ndimi zetu, hatutawahi kumuunga mkono dhalimu
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan alisisitiza kuwa kusimama dhidi ya dhulma ni jambo lililo katika damu ya watu wa Gilgit-Baltistan, na hakuna nguvu yoyote inayoweza kunyamazisha sauti yao ya kudai haki.
-
Ayatollah Ramezani katika Sherehe (Hafla) ya Taklif ya Mabinti wa Senegal: Imani na Elimu ni Mabawa Mawili ya Kuruka (Kupaa) kwa Jamii ya Kiislamu
Kufanyika kwa Sherehe ya Kuvutia ya Taklif (Kufikia umri wa kutekeleza sheria za Kiislamu) kwa Mabinti wa Senegal Huko Dakar sambamba na uwepo wa Ayatollah Reza Ramezani
-
Katika makala maalum ilijadiliwa:
Ustadi wa Kijeshi wa Waislamu wa Yemen ulivyolazimisha Marekani kufikia makubaliano? Hadithi ya Meli za Vita za Marekani - Ghuba ya Uajemi - yatoweka
Leo, Yemen imethibitisha kwa imani kwamba Marekani imepoteza heshima na hadhi yake, na imeweka mwisho kwa hadithi ya meli za kubeba ndege za kivita za Marekani ambazo zilikuwa zikiziogopesha dunia na nchi washindani wao.