Yemen
-
Hezbollah, Ansarullah na Iran Wampongeza Khalil Al-Hayya kwa Kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas
Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, Kata’ib Hezbollah ya Iraq pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran wametoa pongezi kwa Dkt. Khalil Al-Hayya kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti mpya wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas, wakisisitiza kuendelea kwa Mshikamano na Harakati ya Upinzani wa Palestina licha ya kuuawa kwa viongozi wake wakuu.
-
Jeshi la Yemen Latangaza Kuzuia Usafiri wa Baharini wa Saudi Arabia kwa Mujibu wa Kanuni ya “Kuzingira kwa Kuzingira”
Jeshi la Yemen limetangaza kuanza kutekeleza marufuku ya usafiri wa baharini kwa Saudi Arabia, likisema hatua hiyo ni utekelezaji wa kanuni ya “kuzingira kwa kuzingira” na kwamba liko tayari kukabiliana na aina zote za ongezeko la mashambulizi.
-
Pakistan Yaonya Iran: Mashambulizi Dhidi ya Saudi Arabia ni “Mstari Mwekundu”
Pakistan imewasilisha ujumbe kwa Iran kwamba mashambulizi dhidi ya Saudi Arabia, yakiwemo mashambulizi yanayofanywa na harakati ya Ansarullah ya Yemen, yatachukuliwa kuwa mashambulizi dhidi ya Pakistan. Onyo hilo linakuja huku Islamabad ikihofia kuvutwa katika mzozo mpana kati ya Marekani, Iran na washirika wao wa kikanda.
-
Yemen yatangaza kurejesha safari za ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sana'a, yasema imevunja mzingiro
Mamlaka za Yemen zimetangaza kuwa ndege ya Iran itarejea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sana'a na safari za kila siku zitaanza tena, zikisisitiza kuwa zimeamua kuvunja mzingiro na kwamba hakuna nchi itakayozuia haki yao ya kutumia uwanja huo wa ndege.
-
Jeshi la Yemen ladai kuidungua droni ya kivita ya Saudi Arabia katika anga la Al-Baydah
Jeshi la Yemen limedai kuwa limedungua ndege isiyo na rubani ya kivita aina ya Wing Loong-2 UCAV inayodaiwa kumilikiwa na Jeshi la Anga la Saudi Arabia katika anga la mkoa wa Al-Baydah nchini Yemen.
-
Ansarallah yaonya kulenga miundombinu muhimu ya Saudi Arabia katika hatua yake ijayo
Mwanachama wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarallah ya Yemen, Mohammed al-Bukhaiti, amesema kuwa miundombinu muhimu ya Saudi Arabia inaweza kulengwa katika majibu yao yajayo, akieleza kuwa maeneo hayo yanachukuliwa kuwa malengo halali kwa mujibu wa msimamo wa harakati hiyo.
-
Qalibaf: Masharti ya Mazungumzo ya Dhati ni Kuwa Tayari Kikamilifu kwa Vita
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Marekani na utawala wa Kizayuni wamelazimika kutambua nafasi ya washirika wa Iran katika mhimili wa muqawama, akisisitiza kuwa mazungumzo ya kweli hayawezi kufanikiwa bila kuwa na utayari kamili wa kukabiliana na vita.
-
Watafiti wa Yemen na Bahrain: Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Umma Yatakuwa Tukio Kubwa Linalovuka Mipaka ya Ulimwengu wa Kiislamu
Katika mkutano maalumu ulioandaliwa na Shirika la Habari la ABNA kwa anuani ya "Urithi wa Kimkakati na Kistaarabu wa Kiongozi Shahidi wa Umma", watafiti kutoka Yemen na Bahrain walieleza kuwa mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu yatakuwa tukio la kihistoria litakalovutia hisia za ulimwengu mzima na kuleta athari kubwa za kitamaduni na kisiasa.
-
Qaani: Kuanzia Hormuz hadi Bab al-Mandab kutaundwa “ukanda mpya wa kiusalama wa Muqawama”
Kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ismail Qaani, amesema kuwa hatua za wakati muafaka na za “busara” zinazochukuliwa na Yemen zinaonyesha uimara na mshikamano wa mhimili wa Muqawama. Amesema pia kuwa, endapo kutahitajika, pande nyingine zinaweza kujiunga katika hatua hizo.
-
Hadhramaut; Moyo wa Mafuta wa Yemen na Kitovu cha Ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu (UAE)
Mkoa wa Hadhramaut, eneo kubwa zaidi na lenye utajiri mkubwa wa mafuta nchini Yemen, kwa sasa umegeuka kuwa kitovu cha ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu. Licha ya vita vilivyoendelea kwa zaidi ya muongo mmoja, Hadhramaut kwa kiasi kikubwa imeepuka mapigano ya moja kwa moja kati ya serikali ya Yemen iliyojiuzulu na serikali inayoungwa mkono na Harakati ya Ansarullah; hata hivyo, mkoa huu haujaepuka athari za vita na mashindano ya ushawishi wa ndani na kikanda.
-
Araqchi: Umoja wa ardhi na mamlaka ya Yemen lazima vilindwe
Katika mazingira ya kuongezeka kwa mvutano wa kisiasa na kijeshi nchini Yemen, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi, amesisitiza ulazima wa kulindwa umoja wa ardhi na mamlaka ya kujitawala ya nchi hiyo, akionya dhidi ya madhara ya mgawanyiko na kuingilia masuala ya ndani. Kauli hiyo imetolewa kupitia mazungumzo ya simu na mawaziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu, huku pia akigusia hali ya usalama nchini Yemen na kulaani uchokozi unaoendelea wa Israel dhidi ya Lebanon.
-
Kiongozi Mkuu wa Wahouthi: Hatutakubali Israel kutumia ardhi ya Somalia kama kambi ya kijeshi
Ikumbukwe kuwa, moja ya sababu kuu zinazotajwa katika hatua ya Israel kuitambua Somaliland ni nafasi ya kijiografia ya eneo hilo, ambayo inaonekana kuwa na umuhimu wa kimkakati kwa Israel katika kuendesha mashambulizi dhidi ya Wahouthi wa Yemen.
-
-
Mamilioni ya Wayemeni Wafurika Barabarani Kuitetea Qur’ani Tukufu Baada ya Kudharauliwa Nchini Marekani
Qur’ani Tukufu ni Kitabu Kitakatifu kisichoguswa, na kitendo chochote cha kuidharau kitapokelewa kwa upinzani na laana kali kutoka kwa Waislamu duniani kote.
-
Kwa mwaka wa tatu mfululizo; Sudan yaongoza orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani
Sudan kwa mwaka wa tatu mfululizo imeorodheshwa juu kabisa katika orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani.Nchi nyingine zilizoorodheshwa katika ripoti hiyo ni pamoja na: Myanmar, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mali, Burkina Faso, Lebanon, Afghanistan, Cameroon, Chad, Colombia, Niger, Nigeria, Somalia, Syria, Ukraine na Yemen.
-
Hadhramout Yadhibitiwa na Baraza la Mpito la Kusini: Ramani Mpya ya Madaraka Mashariki mwa Yemen
Hadhramout, jimbo kubwa na lenye utajiri mkubwa zaidi nchini Yemen, limeingia rasmi kwenye udhibiti wa Baraza la Mpito la Kusini (STC) baada ya kusonga mbele kwa kasi kwa vikosi vyake. Hatua hii imeufanya mkoa huo kuwa uwanja muhimu wa kuchorwa upya kwa ramani ya madaraka mashariki mwa Yemen.
-
Ushindi wa Jukwaa la Upinzani (Muqawama) ni Kudhihirika kwa Utabiri wa Qur’an
Kushindwa kwa Israel na Marekani katika mapambano ya hivi karibuni kunatokana na uongozi wa busara wa Ayatullah Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Kufungwa kwa Uwanja wa Ndege wa Sana’a kumeweka maisha ya maelfu ya wagonjwa katika hatari
Kwa kuendelea kwa mzingiro na kusitishwa kwa shughuli za Uwanja wa Ndege wa Sana’a, maelfu ya wagonjwa wa Yemen wamenyimwa upatikanaji wa dawa na fursa ya kutibiwa nje ya nchi.
-
Sayyid al-Houthi: Yemen ni nchi ya kwanza katika ulimwengu wa Kiarabu kutengeneza silaha zake za kijeshi
""Dunia sasa imeutambua utawala wa Kizayuni kuwa ni utawala wa kinyama lakini ulioshindwa"
"Hatuwezi kukaa kimya wakati wowote, na kwa namna yoyote hatutafanya biashara au kutoa punguzo juu ya msimamo wetu wa kimsingi wa kiimani, wa jihadi na wa Koran. Taifa letu linatenda kwa mujibu wa maagizo ya Mungu."
-
Waziri wa Ulinzi wa Yemen: Tuko tayari kukabiliana na uvamizi wowote unaoweza kufanywa na adui
“Mohammed Nasser al-Atifi,” Waziri wa Ulinzi wa Serikali ya Sana’a, akitoa pole kwa viongozi wakuu wa nchi kufuatia kuuawa kwa Mkuu wa Majeshi, alisisitiza kuwa: Tuko tayari kikamilifu katika nyanja zote za kijeshi kukabiliana na shambulio au uvamizi wowote unaoweza kutokea.
-
Katika taarifa ya pekee imesema:
"Wanaume majemedari wa Ansarullah wamewaacha Wazayuni katika wasi wasi / Taifa la Yemen linamfufua mataifa yaliyozama usingizini"
“Umma wa Malk Khashab,” Mwanahabari wa kike wa Ansarullah, aliandika: Katika mapambano kati ya wavamizi na Wazayuni dhidi ya Yemen, hesabu zote zimebadilika na mizani imegeuzwa. Kwa hivyo, walianza kulia na kupiga kelele kutokana na wanaume imara wa Yemen na wana-yemen kwa ujumla, na sasa Yemen imekuwa moto wa kuotea mbali na ndoto za kutisha kwao zinazowaamsha mara kwa mara.
-
Falme za Kiarabu, mkono wa Washington na Tel Aviv katika vita ya kijasusi dhidi ya Yemen
Falme za Kiarabu, kwa kubadilisha kambi zake za kijeshi za zamani katika Shabwah na Hadhramaut kuwa vituo vya kijasusi vinavyohusiana na Washington na Tel Aviv, zinacheza jukumu kubwa katika mipango mipya ya ujasusi dhidi ya Yemen.
-
Yemen katika Macho na Moyo wa Sayyid Hassan Nasrallah katika Miaka 11 ya Mapinduzi ya Yemen
Watu wa Yemen katika kumbukumbu ya miaka 11 ya ushindi wa Mapinduzi yao wanapanga kufanya maadhimisho ya kumbukumbu ya Sayyid wa Muqawama, kwa kuwa uhusiano wa Sayyid Muqawama na wananchi pamoja na viongozi wa Yemen ulikuwa ni uhusiano wa pande mbili uliojaa mapenzi na heshima.
-
Hakim: Kimya mbele ya uvamizi wa Israel hakikubaliki
Sayyid Ammar Hakim amesema kuwa ujasiri wa hali ya juu na dharau ya wazi ya utawala wa Kizayuni katika kuvamia nchi za Kiarabu na Kiislamu, na kutenda jinai za kila siku dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Ukingo wa Magharibi, Syria, Lebanon, Yemen, Iran na Qatar ni jambo ambalo kimya dhidi yake hakikubaliki.
-
Hezbollah: Uhalifu wa Wavamizi Dhidi ya Yemen Unaonesha Kiwango cha Kufilisika Kwao
Hezbollah imetoa tamko likisema kuwa: "Uhalifu na mashambulizi yanayofanywa na wavamizi (yaani utawala wa Kizayuni wa Israel) dhidi ya Yemen ni ishara ya wazi ya kufilisika kwao kisiasa, kiakhlaqi na kijeshi."
-
Jeshi la Yemen Lashambulia Tel Aviv kwa Makombora ya “Falastin-2” na “Dhulfikar”
"Adui wa Kizayuni hatapata usalama wala utulivu. Mashambulizi yetu yataendelea kwa kasi kubwa zaidi katika hatua ijayo.”
-
Ayatollah Jannati:
Kwa Umoja wa Umma wa Kiislamu, Ukatili wa Kizayuni Usingeliwezekana / Uuaji wa Viongozi wa Kiyemen Hautaidhoofisha Imani ya Watu wa Yemen
Ayatollah Jannati alilaani vikali shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya mji wa Sana'a, Yemen, ambalo lilipelekea kuuawa kwa Waziri Mkuu na mawaziri kadhaa wa serikali ya mapinduzi ya Yemen.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Dori Najafabadi kwa Watu wa Yemen: "Ushujaa wa Mashahidi Utaimarisha Umoja Dhidi ya Adui wa Kizayuni"
Ninawapa pole familia za mashahidi hawa wapendwa na wananchi wote wa Yemen. Tunawakumbuka mashahidi wote wa Uislamu: kuanzia mashahidi wa tukio la Fakh, mashahidi wa Palestina, Lebanon, na mashahidi wetu wa Iran kama vile Shahidi Qassem Soleimani na wengine.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Akhtari kwa Sayyid Abdul Malik al-Houthi: Shambulio la Israel Nchini Yemen ni Jinai Mpya ya Kivita
"Ninatoa rambirambi zangu za dhati kwa watu wa Yemen mashujaa na kwa uongozi wake jasiri – ukiwemo wewe ndugu yetu mpendwa, Sayyid Abdul Malik – kwa msiba huu mkubwa wa kifo cha Shahidi Ahmad Ghalib al-Rahwi na wenzake waliouawa kwa udhalimu na usaliti wa utawala haramu wa Kizayuni.”
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Lalaani Mauaji ya Kinyama ya Wazayuni Dhidi ya Yemen-Laahidi Jibu Kali kutoka kwa Muqawama wa Kiislam
"Kinyume na matarajio ya Wazayuni na waungaji mkono wao, jinai hizi hazitaweza kudhoofisha irada ya mapambano ya wananchi wa Yemen, bali damu ya mashahidi hawa watukufu itachochea zaidi hasira na mwamko wa upinzani dhidi ya ukoloni na utawala wa Kizayuni kote katika eneo".