Yemen
-
Hakim: Kimya mbele ya uvamizi wa Israel hakikubaliki
Sayyid Ammar Hakim amesema kuwa ujasiri wa hali ya juu na dharau ya wazi ya utawala wa Kizayuni katika kuvamia nchi za Kiarabu na Kiislamu, na kutenda jinai za kila siku dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Ukingo wa Magharibi, Syria, Lebanon, Yemen, Iran na Qatar ni jambo ambalo kimya dhidi yake hakikubaliki.
-
Hezbollah: Uhalifu wa Wavamizi Dhidi ya Yemen Unaonesha Kiwango cha Kufilisika Kwao
Hezbollah imetoa tamko likisema kuwa: "Uhalifu na mashambulizi yanayofanywa na wavamizi (yaani utawala wa Kizayuni wa Israel) dhidi ya Yemen ni ishara ya wazi ya kufilisika kwao kisiasa, kiakhlaqi na kijeshi."
-
Jeshi la Yemen Lashambulia Tel Aviv kwa Makombora ya “Falastin-2” na “Dhulfikar”
"Adui wa Kizayuni hatapata usalama wala utulivu. Mashambulizi yetu yataendelea kwa kasi kubwa zaidi katika hatua ijayo.”
-
Ayatollah Jannati:
Kwa Umoja wa Umma wa Kiislamu, Ukatili wa Kizayuni Usingeliwezekana / Uuaji wa Viongozi wa Kiyemen Hautaidhoofisha Imani ya Watu wa Yemen
Ayatollah Jannati alilaani vikali shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya mji wa Sana'a, Yemen, ambalo lilipelekea kuuawa kwa Waziri Mkuu na mawaziri kadhaa wa serikali ya mapinduzi ya Yemen.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Dori Najafabadi kwa Watu wa Yemen: "Ushujaa wa Mashahidi Utaimarisha Umoja Dhidi ya Adui wa Kizayuni"
Ninawapa pole familia za mashahidi hawa wapendwa na wananchi wote wa Yemen. Tunawakumbuka mashahidi wote wa Uislamu: kuanzia mashahidi wa tukio la Fakh, mashahidi wa Palestina, Lebanon, na mashahidi wetu wa Iran kama vile Shahidi Qassem Soleimani na wengine.
-
Ujumbe wa Rambirambi kutoka kwa Ayatullah Akhtari kwa Sayyid Abdul Malik al-Houthi: Shambulio la Israel Nchini Yemen ni Jinai Mpya ya Kivita
"Ninatoa rambirambi zangu za dhati kwa watu wa Yemen mashujaa na kwa uongozi wake jasiri – ukiwemo wewe ndugu yetu mpendwa, Sayyid Abdul Malik – kwa msiba huu mkubwa wa kifo cha Shahidi Ahmad Ghalib al-Rahwi na wenzake waliouawa kwa udhalimu na usaliti wa utawala haramu wa Kizayuni.”
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Lalaani Mauaji ya Kinyama ya Wazayuni Dhidi ya Yemen-Laahidi Jibu Kali kutoka kwa Muqawama wa Kiislam
"Kinyume na matarajio ya Wazayuni na waungaji mkono wao, jinai hizi hazitaweza kudhoofisha irada ya mapambano ya wananchi wa Yemen, bali damu ya mashahidi hawa watukufu itachochea zaidi hasira na mwamko wa upinzani dhidi ya ukoloni na utawala wa Kizayuni kote katika eneo".
-
Maafisa wa Kiyemeni katika mazungumzo na Abna:
"Madai ya Israel ni udanganyifu na kupindisha mambo ili kufidia udhaifu katika uwanja wa mapambano / Msaada kwa Gaza hautasitishwa"
"Abdulaziz al-Bakr", Katibu Mkuu wa chama cha "Ujamaa wa Kitaaluma wa Kiyemen" na "Hizam al-Asad", mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya harakati ya Ansarullah ya Yemen, katika mazungumzo na shirika la habari la Abna wamesisitiza kuwa: Kila shambulio linalolenga raia wasio na hatia huko Sana'a linageuka kuwa mafuta ya ziada kwa ajili ya harakati ya mapambano ya wananchi wa Yemen.
-
Israel imeushambulia tena Mji Mkuu wa Yemen, Sanaa / Milipuko 10 Mfululizo imetokea katika Mji wa Sanaa
Katika muktadha wa mzozo unaoongezeka kati ya Israel na vikosi vya kijeshi vya Yemen, jeshi la Israel limefanya mashambulizi makubwa ya anga dhidi ya Sanaa.
-
Shambulio Kubwa la Anga la Israel Dhidi ya Mji Mkuu wa Yemen – Ansarullah Yasema Itaendelea Kuunga Mkono Gaza
Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa vyombo vya ujasusi vya Tel Aviv vinaandaa orodha kubwa ya malengo mapya nchini Yemen kwa mashambulizi yajayo.
-
Abdulmalik al-Houthi Awashutumu Waislamu Bilioni Mbili kwa “Kukaa Kimya” Kuhusu Matukio ya Gaza
Katika hotuba yake, al-Houthi alieleza kwa masikitiko na ghadhabu hali ya “kutochukua hatua” kwa Waislamu zaidi ya bilioni mbili duniani, akisema kuwa ukimya huo ni “aibu na fedheha” inayoweza kuleta madhara si tu kwa Palestina, bali pia kwa ulimwengu mzima wa Kiislamu.
-
Jeshi la Yemen Latangaza Awamu ya Nne ya Kufunga Njia za Baharini, Latoa Onyo kwa Ndege Zinazosaidia Israel
Ndege yoyote, iwe ya kijeshi au kibiashara, itakayojihusisha na shughuli za kusaidia Israel, tutaiangamiza. Itaingia kwenye historia.
-
Sayyid Abdul Malik al-Houthi, amesema: "Fungueni njia kuelekea Palestina. Yemen iko tayari Kijeshi kwenda kuisaidia Palestina"
"Huu ni wakati wa Jihad, na taifa letu la Yemen liko tayari kwa mamia ya maelfu ya wapiganaji kuisaidia Palestina.
-
Wataalamu wa Kieneo katika Mahojiano na ABNA: Njaa ya kimfumo dhidi ya watu wa Gaza ni uhalifu usio na kifani na doa la aibu juu ya uso wa Binadamu
Jinai za uharibifu kamili wa ardhi, watu na kila dalili za maisha katika ardhi za Palestina inayokaliwa kwa mabavu (na Utawala wa Kizayuni) zinaakisi matamanio ya jeshi la Netanyahu kuwa tawi la uhalifu wa kimataifa katika ardhi za Kiislamu.
-
Tamko la Maulamaa 100 wa Ulimwengu wa Kiislamu: Trump na Netanyahu ni Maadui wa Mwenyezi Mungu
Marekani na Israel ni wakiukaji wakubwa wa Haki za Binadamu na waendelezaji wa vita visivyo halali dhidi ya Mataifa ya Kiislamu (Palestina, Yemen, Lebanon, Iraq, Iran n.k).
-
Msemaji wa Jeshi la Yemen: "Tumeushambulia Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion"
Operesheni za Yemen zitaendelea hadi vita na mzingiro dhidi ya Gaza utakapositishwa.
-
Wananchi wa Yemen wanalenga (wanashambulia) maeneo mbalimbali ya Wazayuni kujibu jinai zinazoendelea kufanywa na Israel
Vikosi vya jeshi la Yemen vimeanzisha operesheni mpya ya ndege zisizo na rubani dhidi ya utawala wa Israel, hatua ambayo kwa mujibu wa duru za Yemen, ilifanyika kujibu mauaji ya raia huko Gaza.
-
Mafanikio mawili ya Yemen ndani ya siku moja; Mashambulizi ya Kimaonyesho dhidi ya Hodeidah yazimwa na kushindwa/Meli "Magic Seas" Yazamishwa Baharini
Yemen, imefanikiwa kuitwanga meli iliyokuwa ikielekea maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na utawala haram wa Kizayuni, na kuizamisha baharini.
-
Yemen: Ikiwa Marekani itaingia vitani dhidi ya Iran ili kuisaidia Israel, tutashambulia Meli zake katika Bahari Nyekundu
"Yemen haitasalia kuishia kutizama na kutojali uchokozi wowote dhidi ya nchi ya Kiislamu."
-
Taarifa kutoka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kuhusu Wimbi la 17 la Mashambulizi Mchanganyiko dhidi ya Utawala wa Kizayuni
Vituo hivi vimekuwa kitovu cha uovu dhidi ya wadhulumiwa wa Gaza, Lebanon, Yemen, na pia katika vita vilivyowekwa kwa uchokozi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran tangu Kimbunga cha Al-Aqsa kilipoanza.
-
Kiongozi cha Ansarullah Yemen:
"Jinai dhidi ya Iran hata bada ya kusisitiza kuwa haina haja ya silaha za Nyuklia ni kwa sababu ya misimamo imara Iran juu ya kadhia ya Palestina"
Wamagharibi hatwaki kuona Iran ikiwa ni nchi huru, na hii ni kutokana na msimamo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kuwatetea wananchi wa Palestina na kukataa udhalimu wa uvamizi wa Kizayuni kwa ardhi za Taifa la Palestina.
-
Ansarullah: Operesheni za Kijeshi za Yemen Zitaendelea Kuongezeka Taratibu
Mwanachama wa Ofisi ya Kisiasa ya Ansarullah Yemen amesisitiza kuwa ikiwa uvamizi wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza utaendelea, basi operesheni za kijeshi za Yemen zitaendelea kuongezeka taratibu.
-
Huthi: Ziara ya Donald Trump katika Nchi za Kiarabu Ilikuwa kwa Ajili ya Kudai Hongo
Mwanachama wa Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen, Mohammed Ali al-Houthi, amesema kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zimeathiriwa na udhaifu wa kisaikolojia na shida ya kushindwa. Aliongeza kuwa nchi hizi haziwezi hata kukata uhusiano wa kidiplomasia na Israeli, jambo ambalo linaonyesha upungufu wa msimamo na ushupavu katika kushikilia mikao ya kisiasa.
-
Katika makala maalum ilijadiliwa:
Ustadi wa Kijeshi wa Waislamu wa Yemen ulivyolazimisha Marekani kufikia makubaliano? Hadithi ya Meli za Vita za Marekani - Ghuba ya Uajemi - yatoweka
Leo, Yemen imethibitisha kwa imani kwamba Marekani imepoteza heshima na hadhi yake, na imeweka mwisho kwa hadithi ya meli za kubeba ndege za kivita za Marekani ambazo zilikuwa zikiziogopesha dunia na nchi washindani wao.
-
Dola bilioni 8: Gharama ya kashfa (fedheha) na mashambulizi yaliyoshindwa ya Marekani nchini Yemen
Vyombo vya habari vya Marekani vimekadiria gharama ya mashambulizi ya nchi hiyo dhidi ya Yemen, katika muktadha wa kuunga mkono Israel, kufikia dola bilioni 8. Vimeripoti kuwa Trump alikuwa akimkejeli Biden kwa sababu ya gharama za vita dhidi ya Yemen, lakini yeye mwenyewe alisababisha hasara kubwa zaidi, huku Serikali ikificha takwimu halisi za vifo.
-
Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu: Kundi la Mwenyezi Mungu, linalomtii Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na waliokuwa Waumini wa kweli, Hao ndio washindi wa kweli
"Hezbollah" humaanisha: Kundi lililojifunga na miongozo ya Mwenyezi Mungu, linalosimama na kutetea haki, hata likiwa ni dogo au linakabiliwa na maadui wakubwa. Aya hii imekuwa nembo ya Harakati za Muqawama (Upinzani wa Kiislamu) kama vile Hezbollah ya Lebanon, Ansarullah ya Yemen, na wengineo wanaopambana dhidi ya dhulma ya mabeberu ya Kimataifa.
-
Kushindwa kwa Wamarekani Mbele ya Msimamo wa Wayemen Katika Kipindi cha Siku 50 / Ansarullah Yabadilisha Mlinganyo wa Dunia kwa Manufaa ya Muqawama
Katika kipindi cha siku 50 za mapambano ya kistratejia baharini, harakati ya Ansarullah ya Yemen imeweza kusimama imara dhidi ya mashinikizo ya kijeshi na kisiasa ya Marekani na washirika wake, na hatimaye kuwadhihirishia ulimwengu kwamba dhamira ya mataifa huru inaweza kuvunja nguvu za mabeberu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: "Hakuna manufaa yoyote kwa Umma wa Kiislamu yaliyo juu ya Umoja"
Kiongozi Muadham wa Mapinduzi ameeleza katika Mkutano na wahusika wa Hajj na baadhi ya Waumini waliotembelea Nyumba Tukufu (Al-Kaaba) kwamba: "Muundo na sura ya nje ya ibada hii ni ya kisiasa kabisa, lakini maudhui ya vipengele vyake ni ya kiroho na ya ibada, ili manufaa ya Wanadamu wote yaweze kutimizwa. Na leo, faida kubwa kwa Umma wa Kiislamu ni 'Umoja na Ushirikiano' ili kutatua matatizo ya Ulimwengu wa Kiislamu. Ikiwa umoja huu ungelikuwepo, matatizo kama ya Gaza na Yemen yasingekuwepo."
-
Yemen yaachia kombora la Hipersoniki kulenga kituo cha kijeshi cha Wazayuni katika eneo la Negev
Jeshi la Missili la Jeshi la Silaha la Yemen limetekeleza operesheni ya kijeshi ikilenga Kituo cha Anga cha Nevatim katika eneo la Negev, kusini mwa Palestina iliyokaliwa, kwa kutumia kombora la hipersoniki la balistiki.
-
Kushindwa kwa Marekani nchini Yemen kumezusha wasiwasi miongoni mwa nchi za Kiarabu. Nini kitatokea ikiwa San'a itakuwa Mamlaka yenye Nguvu Kikanda?
Kwa kuzingatia chaguzi ndogo za Amerika, mashaka yameongezeka miongoni mwa maadui wa Yemen katika nchi za Ghuba ya Uajemi, na hii imefanya kazi ya vyombo vyao vya habari - ambavyo vinaendana kikamilifu na (riwaya) simulizi ya Marekani na Israel - kuwa ngumu; Hadi wanakimbilia kuwatuhumu “Ansarullah” kwa kutumia vita vibaya.