serikali
-
Iran Yatahadharisha Dhidi ya Kutumiwa kwa Maeneo Matakatifu Kuchochea Migogoro
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, atoa wito wa tahadhari kuhusu madai ya kuzuiwa kwa droni iliyokuwa ikielekea Makka.
-
Serikali ya Iran Yalaani Mashambulizi dhidi ya Raia Sereki na Kuyataja kuwa Ukiukaji Mkubwa wa Sheria za Kimataifa
Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani mashambulizi yaliyowalenga raia katika eneo la Sereki, kusini mwa Iran, ikisema kuwa mashambulizi hayo pamoja na shambulio la awali dhidi ya shule ya Minab, lililosababisha vifo vya wanafunzi, ni ukiukaji mkubwa wa misingi ya kibinadamu na sheria za kimataifa.
-
Kwa nini Hizbullah ya Lebanon ilikataa kukabidhi maeneo ya miinuko ya Ali al-Taher?
Pendekezo ambalo kwa msingi wake Hizbullah ingeyaondoa majeshi yake katika maeneo ya miinuko ya Ali al-Taher na Jeshi la Lebanon kuchukua nafasi yake, kwa mtazamo wa Hizbullah si mpangilio wa kijeshi wa uwanjani tu, bali linaweza kuunda mfano wa kulazimisha madai zaidi ya utawala wa Kizayuni katika maeneo mengine ya Lebanon.
-
Mpango Mpya wa Jimbo la Tamil Nadu, India, wa Kurahisisha Masomo ya Vyuo Vikuu kwa Wanawake Waislamu
Serikali ya Jimbo la Tamil Nadu nchini India imetangaza kwamba italipia ada za masomo ya chuo kikuu kwa wanawake Waislamu wanaokidhi vigezo.
-
Taliban yakosoa kuondolewa kwa Afghanistan katika mkutano wa Shanghai
Zabihullah Mujahid amesema kuwa maamuzi ya kikanda ya Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai bila ushiriki wa Afghanistan yatakuwa “hayajakamilika”; wakati huohuo, viongozi wa jumuiya hiyo katika mkutano wa Bishkek kwa mara nyingine wamesema kuwa kuundwa kwa serikali jumuishi nchini Afghanistan ni sharti la kufikiwa kwa amani na utulivu wa kudumu.
-
Kiongozi wa Iran Asisitiza Umoja wa Kitaifa na Kulinda Mshikamano wa Kijamii
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, amesisitiza umuhimu wa serikali na taasisi zote za nchi kulinda umoja wa kitaifa na mshikamano wa kijamii, akionya dhidi ya kauli zinazoweza kuchochea mgawanyiko miongoni mwa wananchi.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Kufanya chochote kinachodhuru mshikamano wa kijamii ni marufuku
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Husseini Khamenei, amesisitiza umuhimu wa kudumisha umoja na mshikamano wa kijamii nchini Iran, akitangaza kwa uthabiti kwamba hatua au kauli yoyote inayodhuru mshikamano wa jamii ni marufuku. Aidha, ametoa wito wa kuimarisha uchumi wa ndani, kutumia teknolojia na ubunifu wa vijana, pamoja na kusimamia utamaduni, elimu na malezi kwa lengo la kuijenga Iran yenye nguvu zaidi.
-
Kesi ya Mufti wa Zamani wa Syria Yakabiliwa na Hukumu; Waendesha Mashtaka Wadai Adhabu ya Kifo
Kesi ya Ahmad Badr al-Din Hassoun, Mufti Mkuu wa zamani wa Syria, imeingia hatua ya mwisho baada ya kikao cha tano katika Mahakama ya Jinai ya Nne mjini Damascus. Waendesha mashtaka wamewahi kuomba apewe adhabu ya kifo kwa tuhuma za kuchochea vurugu na kuunga mkono ukandamizaji wa serikali iliyopita, huku tarehe 24 Agosti ikiwekwa kwa ajili ya mapitio ya mwisho na kutolewa kwa hukumu.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Kuunga mkono Vikosi vya Ulinzi ni wajibu na jukumu la kulinda usalama wa nchi
Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuunga mkono Vikosi vya Ulinzi ni wajibu na jukumu la serikali katika kuhakikisha usalama wa nchi, akisisitiza kuwa msaada huo unahusisha mahitaji ya ulinzi, kuboresha hali za wanajeshi na familia zao, pamoja na kuimarisha uratibu na taasisi za ulinzi.
-
Rais Pezeshkian Ampongeza Meja Jenerali Ali Abdollahi kwa Kuteuliwa Kuwa Mkuu wa Wafanyakazi wa Majeshi ya Iran
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amempongeza Meja Jenerali wa Anga Ali Abdollahi kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Wafanyakazi wa Majeshi ya Iran, akisisitiza umuhimu wa kuimarisha uratibu wa vyombo vya dola na kuongeza uwezo wa kuzuia vitisho wa nchi.
-
Baqaei: Uamuzi kuhusu hati ya Mkataba wa Hali ya Kisheria ya Bahari ya Caspian ni jukumu la Bunge la Iran
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amesema uamuzi kuhusu hati ya Mkataba wa Hali ya Kisheria ya Bahari ya Caspian uko chini ya mamlaka ya Bunge la Iran, baada ya kukamilika kwa mchakato wa kuichunguza na kwa mujibu wa Katiba ya nchi.
-
Urithi wa Shahidi Nasirzadeh: Nguzo ya Usalama na Ulinzi wa Iran
Katika kuelekea Wiki ya Serikali nchini Iran, urithi wa mashahidi na watumishi wa taifa unakumbusha umuhimu wa kuchukulia dhamana ya uongozi kama amana ya Mwenyezi Mungu, na kutumia uwezo wote katika kulinda heshima, usalama na maslahi ya taifa.
-
The Guardian: Mtandao wa X Watuhumiwa Kuwazuia Wakosoaji wa Serikali ya Saudi Arabia
Gazeti la The Guardian linaripoti kuwa mtandao wa kijamii wa X umezuia zaidi ya akaunti 60 zinazoukosoa serikali ya Saudi Arabia kwa watumiaji walioko ndani ya nchi hiyo, hatua iliyozua ukosoaji kutoka kwa watetezi wa haki za binadamu.
-
Jeshi la Serikali ya Yemen Lazindua Droni Mpya za "Eiban" na "Naqm" kwa Mashambulizi ya Njia Moja
Jeshi la Serikali ya Yemen inayotambuliwa kimataifa limetangaza uzinduzi wa droni mbili mpya za mashambulizi ya njia moja, "Eiban" na "Naqm", hatua inayoashiria kuendelea kwa ushindani wa teknolojia za kijeshi nchini humo huku kukiwa na mjadala kuhusu matumizi ya droni za gharama nafuu katika vita vya kisasa.
-
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Nchi zinazosaidia mchokozi zitapokea jibu kali
IRGC imetahadharisha kuwa nchi zinazosaidia Marekani zinaweza kukabiliwa na jibu kali iwapo hazitabadilisha mwenendo wao. Pia imesema vikosi vya majini vya Iran vina udhibiti wa Mlango wa Hormuz, ambao Iran inasema utaendelea kufungwa huku vitisho na uingiliaji wa Marekani katika eneo hilo vikiendelea. IRGC imeonya kuwa hatua hizo zinaweza kuongeza zaidi mvutano na kuzidisha hali ya usalama katika eneo.
-
Iraq yakemea mashambulizi ya anga ya Marekani na Saudi Arabia
Serikali ya Iraq imelaani mashambulizi ya Marekani na Saudi Arabia, ikisisitiza kuwa yanakiuka mamlaka yake. Baraza la Usalama wa Taifa limeagiza kuandaliwa kwa mpango wa kukabiliana na ukiukaji huo, huku Wizara ya Mambo ya Nje ikitakiwa kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Iraq pia imeahidi kurekodi matukio hayo na kulinda haki na mamlaka yake ya kitaifa.
-
Muqawama wa Kiislamu Iraq: Jibu kwa Marekani Halitakwepeka Baada ya Arbaeen, Yatoa Onyo kwa Serikali ya Iraq
Muqawama wa Kiislamu nchini Iraq umetangaza kuwa utatoa jibu dhidi ya kile ulichokiita mashambulizi ya Marekani baada ya kumalizika kwa ibada za Arbaeen ya Imam Hussein (as), huku ukitoa muda kwa serikali ya Iraq hadi tarehe 23 Safar kuchukua msimamo kuhusu usalama na suala la silaha za makundi ya Muqawama.
-
Iraq Yapokea Zaidi ya Mazuwwari Milioni 1.8 kwa Ajili ya Ziara ya Arbaeen ya Imam Hussein (a.s)
Zaidi ya mahujaji milioni 1.813 wameingia Iraq tangu mwanzo wa mwezi wa Muharram. Mahujaji hao wametoka katika mataifa 172 duniani kushiriki Ziara ya Arbaeen ya Imam Husayn (a.s). Mamlaka za Iraq zimesema maandalizi ya kiusalama na huduma kwa mahujaji yanaendelea katika maeneo mbalimbali ya nchi.
-
Mamlaka ya Palestina: Serikali ya Netanyahu Inawajibika Kikamilifu kwa Kuongezeka kwa Mvutano Katika Ukingo wa Magharibi
Mamlaka ya Palestina imeishutumu serikali ya Netanyahu kwa kuhusika kikamilifu na uhalifu wa kila siku unaofanywa na walowezi wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina, huku ikionya kuwa upanuzi wa makazi ya walowezi na kuongezeka kwa hatua za kijeshi kunaweza kuusukuma Ukingo wa Magharibi kuelekea mlipuko mkubwa wa hali ya mambo.
-
Zaidi ya Raia 30 Wauawa Kufuatia Mashambulizi Kusini mwa Iran, Serikali Yalaani Vikali
Serikali ya Iran imelaani vikali mashambulizi yaliyolenga maeneo ya kusini mwa nchi, yakisababisha vifo vya zaidi ya raia 30, huku ikithibitisha kuwa huduma muhimu na misaada kwa wananchi katika maeneo yaliyoathirika vinaendelea bila kusitishwa.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Umoja Ndio Urithi Mkuu Aliouacha Imam Shahidi kwa Iran na Ulimwengu wa Kiislamu
Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuwa umoja ndio urithi muhimu zaidi aliouacha Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei kwa Iran na ulimwengu wa Kiislamu, akisisitiza kuwa tofauti za maoni hazipaswi kuudhoofisha urithi huo wa thamani.
-
Video ya Kifo cha Mfungwa Mweusi Marekani Yafichua Matumizi ya Nguvu Kupita Kiasi na Walinzi wa Gereza
Mahakama ya jimbo la Connecticut nchini Marekani imetoa video inayoonyesha jinsi mfungwa Mmarekani mwenye asili ya Afrika, J'Allen Jones, alivyofariki baada ya kudhibitiwa kwa nguvu na walinzi wa gereza, jambo lililozua maswali mapya kuhusu ukatili ndani ya magereza ya Marekani.
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Jeshi la Iran: Tuko tayari kutekeleza amri za Kiongozi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na kujibu ukiukaji wowote wa adui
Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuwa vikosi vyake vipo katika hali ya utayari wa juu, vikiwa “na mikono kwenye vichocheo vya silaha na masikio yakisubiri amri za Kiongozi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi,” likisisitiza kuwa litailinda Iran na maslahi yake endapo upande wa adui utakiuka makubaliano yaliyofikiwa.
-
Rais Pezeshkian: Juhudi za Pakistan Zitabaki Kwenye Kumbukumbu ya Wairan Milele
Rais wa Iran ameipongeza Pakistan kwa juhudi zake za dhati katika upatanishi uliochangia kufikiwa kwa makubaliano ya awali ya kumaliza vita, huku Tehran na Islamabad zikiahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kwa ajili ya amani na maendeleo ya kikanda.
-
Serikali ya Iran Yatangaza Mali Zilizoachwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (r.a)
Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema uchunguzi wa mali za Ayatullah Sayyid Ali Khamenei (r.a.) umebaini kuwa aliacha mali chache sana, jambo linalotajwa kuakisi maisha yake ya ucha-Mungu na kujiepusha na anasa.
-
Makundi ya Muqawama Iraq Yalionya Serikali ya Mpito ya Syria Dhidi ya Ushirikiano na Marekani na Israel
Makundi ya Muqawama nchini Iraq yametoa onyo kali kwa serikali ya mpito ya Syria, yakisema kuwa ushirikiano wowote wa kijeshi au kiusalama na Marekani na Israel dhidi ya Hizbullah ya Lebanon utakabiliwa na jibu la kijeshi.
-
Sheikh Pro.Alhad Mussa Salum: Serikali Hupambana na Kuchukua Hatua dhidi ya Wanaotishia Maslahi Yake, Sio kwa Msingi wa Dini
Sheikh Prof.Alhad Mussa Salum: "Nchi ya Tanzania ni nchi ya Amani na sisi sote ni Watanzania, tunaishi kwa Upendo na Amani na watu wote. Uislamu ni Amani na unatufundisha kuishi kwa wema na watu wote."
-
Burkina Faso Yakanusha Taarifa za Machafuko; Serikali Yatetea Muswada wa Kudhibiti Maeneo ya Ibada
Serikali ya Burkina Faso imetetea hatua ya kumkamata mwanazuoni wa Kiislamu Dk. Mohamed Kindou kufuatia hotuba yake kuhusu muswada wa maeneo ya ibada, huku ikisisitiza kuwa hakuna uasi dhidi ya Rais Ibrahim Traoré na kwamba wananchi bado wanaunga mkono uongozi wake.
-
Rais wa Venezuela Nicolás Maduro Aripotiwa Kuhamishwa Kwenye Mahakama ya Jiji la New York +Picha
Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro, ameripotiwa kuhamishwa siku ya Jumatatu kwenda katika mahakama ya Jiji la New York kwa ajili ya hatua za kisheria zinazohusiana na tuhuma zinazomkabili. Tukio hilo limeibua mjadala mpana wa kimataifa kuhusu athari zake za kisiasa na kidiplomasia.